Sunday, May 20, 2012

DROGBA AIPA CHELSEA UBINGWA KLABU BINGWA ULAYA!

Mmiliki wa Kalbu ya Chelsea Abahamovich akinyanyua kombe
Mashujaa wa jana Didier drogba na Kipa Peter Cech.

ALLIANZ ARENA, MUNICH,UJERUMANI, Hatimaye Chelsea wamefanikiwa kufuta machozi na maumivu waliyoyapata miaka minne iliyopita katika fainali za UEFA baada ya hapo leo kufanikiwa kutwaa kombe klabu bingwa Ulaya.

Alikuwa ni yule yule mkongwe aliyetegemewa Didier Drogba ndiye aliyeiongoza timu yake kutwaa ubingwa baada ya kufunga goli la kusawazisha na lile la ushindi katika Penati ya mwisho.

Buyern Munich ndiyo walikuwa wa kwanza kuliona lango la Chelsea katika dakika ya 83 kupitia kwa Thomas Muller, lakini dakika tano baaadaye katika dakika ya 88 Drogba akaisawazishia timu yake goli hilo kupitia mpira wa kichwa.
Thomas Muller akifunga goli.



Drogba akifunga goli la Kusawazisha kwa Chelsea.

Baada ya dakika 90 kuisha matokeo yalibaki kuwa 1-1 na hata baada ya Dakika 30 kuongezwa bado hali ilibaki hivyo na ndipo walipoingia katika mikwaju ya penati.


Katika Mikwaju hiyo Bayern ndiyo walikuwa wa kwanza kupiga ambapo ilikuwa kamifuatavyo:

 Philipp Lahm   alifunga, akafuata Juan Mata(Chelsea)-Akakosa, akafuata Mario Gomez(Bayern Munich)-akafunga, akfuata David Luiz(Chelsea)-akafunga, Manuel Neuer(Bayern)-akafunga,Frank Lampard(Chelsea) -akafunga, Ivica Olic(Bayern)-akakosa,Ashley Cole (Chelsea)-akafunga, Bastian Schweinsteiger (Bayern)-akafunga, na kisha Didier Drogba(Chelsea) -akafunga penati ya Ushindi.


Chelsea wakishangilia baada ya Penati ya mwisho.

Wachezaji wa Bayern wakigugumia kwa machungu.

No comments:

Post a Comment