Thursday, May 3, 2012

UJUMBE WA BAN KI- MOON KUADHIMISHA SIKU YA UHURU WA VYOMBO VYA HABARI DUNIANI:


Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw Ban Ki-moon akiwa  na Mkurugenzi  Mkuu wa UNESCO Bi Irina Bokova kwa katika kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani .

 

 

Katika kipindi hiki cha mabadiliko ya kasi na yenye nguvu, uhuru na uongezekaji kwa wingi wa vyombo vya habari sio suala linalozuilika.

 

 Mwaka uliopita mapinduzi huko Afrika kaskazini na mashariki ya kati, pia katika mitandao ya kijamii,simu na satelaiti yamefanya kazi kubwa kutengeneza mlolongo wa mabadiliko kutoka kwa muuza mboga za majani masikini aliyekuwa analilia utu wa kibinadamu mpaka kuanguka kwa tawala za kidiktekta na kuleta uwezekano wa mamilioni ya watu kwa mara ya kwanza kufurahia demokrasi na nafasi walizokuwa wakinyimwa.

 

 Hiyo ndiyo inayoelezewa kama dhima iliyobeba ujumbe wa uhuru wa vyombo vya habari mwaka huu; Sauti mpya: Uhuru wa vyombo unasaidia kubadilisha jamii.

 

Chombo huru cha habari kinawapa watu taarifa wanazozitaka ili kufanya maamuzi muhimu kuhusu maisha yao. Pia kinawawajibisha viongozi na kuweka wazi rushwa, kuongeza uwazi katika maamuzi. Pia chombo huru cha habari kinafungua ufahamu na kutoa matokeo ya sauti mbalimbali hasa zile ambazo pengine zisingesikika.

 

Lakini uhuru wa vyombo vya habari bado umebakia wenye uchungu.kila siku waandishi wa habari  wanapo fanya kazi zao wanakutana na vitisho vyenye kuogofyaa. Mwaka uliopita zaidi ya waandishi 60 waliuawa duniani kote, na wengine wengi kujeruhiwa.Kama kwa mujibu wa kamisheni ya kuwalinda waandishi wa habari mpaka Desemba, 1 mwaka jana kuna waandishi 179 wa habari walikuwa wakizuiliwa.Hiyo ni sawa na ongezeko la asilimia 20 zaidi ya mwaka 2010, na kubwa zaidi tangu 1990.

Idadi nyingine kubwa ya waandishi wa habari walifungiwa na kunyamazishwa na serikali, mashirika na watu wenye nguvu.huku uhuru kwa wale wanaowashambulia waandishi wa habari ukionekana wazi.


 Nina wasiwasi kuwa mashambulizi dhidi  ya waandishi wa habari yapo yanakua kwa sasa. Natoa wito kwa wahusika wote kuzuia na kuzichukulia hatua za kisheria vurugu hizi. Watetezi wa uhuru wa vyombo vya habari wanatetea haki zetu sisi ni lazima tulinde zao pia.


Mwezi wa eptemba mwaka jana umoja wa mataifa uliitisha kwa mara ya kwanza mkutano wa wadau kuhusu usalama wa waandishi wa habari.mkutano ulizaa mpango kazi dhabiti, na mfumo wa umoja wa mataifa kwa sasa unakusanya na kuimarisha nguvu zetu kuongeza ufahamu juu ya mambo haya, unasaidia  wanachama kuimarisha mifumo ya kisheria na kuwashawishi kuchunguza visa vya mashambulio dhidi ya waandishi.

 

 Tunapoadhimisha siku ya Uhuru wa vyombo vya habari, tuhaidi kufanya kila linalowezekana kuhakikisha waandishi wanafanya kazi zao katika mazingira mapya na ya yenye kuendana  na uandishi ..... ambayo yataleta mchango muhimu katika jamii Imara,yenye afya na yenye amani zaidi

No comments:

Post a Comment