Friday, May 18, 2012

MKUTANO WA G8 WAANZA:

 MAREKANI, Mkutano wa nchi tajiri za kwa viwanda umeanza hapo jana huko Camp David,Maryland, Marekani ambapo moja ya Ajenda muhimu ni usalama wa chakula Afrika na hali ya uchumi ulaya hasa katika nchi zenye migogoro ya kiuchumi ikiwemo Uturuki na Ugiriki.
Mkutano huo wa siku mbili unawakutanisha viongozi wa Uingereza,Ufaransa,Ujerumani,Italia,Japan,na Marekani ambaye ni mwenyeji wa mkutano huo.

Moja ya ajenda katika mkutano ni pamoja na Hali ya uchumi Ulaya, Hali ya nyuklia Iran, Hali ya Syria, Pia usalama wa chakula na nishati duniani ikiwemo Afrika.

Hata hivyo licha ya ajenda hizo bado wengi hawana matumaini na mkutano huo kwani iliyotangulia haikuzaa matunda kama ilivyotegemewa.

No comments:

Post a Comment