Friday, May 18, 2012

MPENDWA PATRICK MAFISANGO AAGWA TCC.

Mwili wa mafisango Ukiwa Umebabwa na wachezaji wenzake.
Juma Kaseja Akilia Kwa uchungu.
Mdogo wa marehemu Akisaidiwa baada ya kuishiwa nguvu.
Kocha wa Simba Milovan.
Dar Es Salaam, Mwili wa aliyekuwa mchezaji wa Simba na timu ya taifa ya Kongo, Patrick Mutesa Mafisango umeagwa rasmi katika viwanja vya TCC Chng'ombe Jijini dar es Salaam,na mamia ya wanamichezo wakiongozwa na waziri wa michezo Dr.Fennela Mukangala.

Waombolezaji wengine(Picha zote kwa hisani ya millardayo.com na Global Publishers)
Wengi wa mashabiki na wapenzi hao wa soka walionekana kuwa na majonzi huku wachezaji wenzake,pamoja na kocha wa Timu ya Simba Milovan wakishindwa kujizuia kwa machozi.

mwili wa mafisango umesafirishwa jioni ya Ijumaa hii kuelekea nyumbani kwao Nchini Kongo kwa ajili ya mazishi yatakayofanyka siku ya Jumapili mchana.

Patrick mafisango mchezaji wa timu ya Simba na Timu ya taifa ya Kongo alikuwa mfungaji namba tatu wa ligi kuu ya Vodacom msimu huu na alikuwa na msaada mkubwa katika kufanikisha Timu ya Simba kupata ubingwa Msimu huu, Anga za Kimataifa Inaungana na wadau wote wa Michezo pamoja na familia ya marehemu Kumuombea heri ; MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALA PEMA PEPONI, AMEN.

No comments:

Post a Comment