Sunday, May 13, 2012

NI MANCHESTER CITY!!


Manchester-UINGEREZA,
Magoli mawili ya dakika za nyongeza yameileta miujiza isiyokuwa ikitegemewa na wengi na kuifanya timu ya Manchester City kutwaa ubingwa wa ligi kuu ya Uingereza tangu mwaka 1968. Magoli ya  Edin Dzeko na Sergio Aguero dhidi ya QPR katika dakika za nyongeza yalifufua matumaini ya Manchester City ambayo mpaka dakika 90 ilikuwa nyuma kwa goli moja. Mpaka mapumziko Manchester city walikuwa wakiongoza kwa goli moja la Zabaleta, lakini mambo yalibadilika katika kipindi cha pili baada ya Mchezaji wa QPR Cisse kusawazisha kabla ya Mackie kuongeza goli la pili kwa QPR akimalizia kwa kichwa krosi safi kutoka kwa Traore.

Manchester City wamekuwa mabingwa wapya baada ya kufikisha pointi 89 sawa na mahasimu wao wakubwa Manchester United lakini wao wapo mbele kwa magoli.

Bidii binafsi za wachezaji Yaya Toure na Balotel zilioonekana dhahiri kuzaa matunda kwa timu hiyo.

Huko ujerumani nako timu ya Borushia Dotmund ndio mabingwa wapya wa ligi kuu ya nchi hiyo.

No comments:

Post a Comment