Tuesday, May 29, 2012

MLIPUKO MKUBWA WATOKEA TENA KENYA!

NAIROBI,KENYA, Mlipuko mwingine umetokea sehemu yenye maduka mengi  katikati ya jiji la Nairobi karibu na Chuo kikuu cha Mount Kenya na kujeruhi watu wapatao 16 kwa mujibu wa  polisi.
habari zilizotolewa leo na chanzo cha polisi zimesema mlipuko huo umetokana na bomu.
Mlipuko mkubwa ulitokeamnamo saa 7:10 mchana saa za Afrika mashariki katika moja ya majengo yaliyopakana na maghorofa maeneo hayo , baadhi ya mashuhuda wamesema wanamhisi mtu aliyekuwa na begi aliyekuwa akija na kuondoka  eneo hilo.
Majeruhi walionekana wakipewa huduma na watu wa afya ambao walijaribu kuwaondoa mamia waliokusanyika katika eneo hilo kama mashuhuda.Picha za televisheni za Kenya zilionesha moshi mkubwa ukitoka katikakati ya majengo hayo.
Ingawa bado haijathibitka imeaminiwa kuwa kundi la kigaidi la nchini Somalia la Al-Shabab limehusika na mlipuko huo.Kundi hilo liliahidi na limehusika kutekeleza mashambulio kama hayo yaliyotokea nchii humo hivi karibuni, baada ya serikali ya Kenya kuingia nchini Somalia kwa lengo la kuendesha operesheni ya kulisambaratisha kundi la Al-Shabab.

No comments:

Post a Comment