Friday, May 18, 2012

MKURUGENZI WA TBS ASIMAMISHWA KAZI.

Mkurugenzi wa TBS Charles Ekerege.
 Dar es Salaam, Siku chache baada ya kuteuliwa waziri wa viwanda Mh.Abdallah Kigoda ametoa maagizo ya kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi mkuu wa shirika la Viwango tanzania TBS Bw Charles Ekelege. Akiongea na waandishi wa habari hapo juzi Waziri kigoda amesema Moja ya sababu za rais kuamua kuvunja baraza la mawaziri lililokuwepo ni pamoja na tuhuma nzito zilizokuwa zikielekezwa TBS hivyo ni vyema mkurugenzi huyo akasimamishwa kupisha uchunguzi na hatua zaidi za kisheria.


Wachunguzi wa mambo wanahisi hiyo ni sehemu ya ahadi alizotoa rais Kikwete katika hotuba yake siku alipokuwa akitangaza baraza jipya la Mawaziri ambapo aliahidi kuwawajibisha watendaji wa ngazi za chini pia ambao mara nyingi ni chanzo cha mawaziri kuwajibika.

Imekuwa ni kawaida kwa watendaji wengi wa ngazi za chini katika wizara kuzembea kwa kuelewa kuwa wao sio wawajibikaji wa moja kwa moja zitokeapo tuhuma pengine hatua hizi zitasaidia.

No comments:

Post a Comment