Tuesday, March 4, 2014

Luis Suarez asaini mkataba mpya


 
Everton ikiwa mbele ya Chelsea, katika michuano ya ligi kuu ya Uingereza, baada ya kuifunga Swansea mabao (2-1), na kuipa shinikizo the Bleus ambayo itakwaruzana na Arsenal leo jumatatu. Tottehnam imefungwa na Southampton mabao (3-2).
Chelsea ambayo ilishapoteza mara moja msimu huu, imekua na shauku toka tarehe 5 mwezi oktoba kusogea mbele ikitoka kwenye nafasi ya 4. Chelsea ina alama 34, ikiwa mbele ya Arsenal alama 1.
Liverpool kwa sasa ndio inaongoza.



Hata hivo, Mshambuliaji mahiri wa Klabu ya Liverpoool Luis Suarez amesaini mkataba kuendelea kusakata gozi kwenye Klabu hiyo ya Liverpool.

Awali mkataba wa Suarez ambaye alijiunga na klabu hiyo January 2011 na akiwa tayari amekwishafunga mabao 17 msimu huu, ulitaraji kukamilika mwaka 2016.

Luis Suarez, mwenye umri wa miaka 26, amesema amefurahi kufikia makubaliano ya kuendelea kuitumikia kwa muda mrefu klabu hii ya Liverpool, akibaini kwamba timu hio ina wachezaji mahiri, na inazidi kuimarika kila wakati.

Naye kocha mkuu wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers ameuambia mtandao wa klabu hiyo kuwa hiyo ni habari njema kwa kila mdau wa Klabu ya Liverpool, wakiwemo wamiliki wa klabu lakini muhimu Zaidi Mashabiki wa klabu hiyo.

“Suarez ni mchezaji wa kiwango cha dunia, mwenye kipaji cha hali ya juu, na kwa kuendelea kuwa naye wakati huu ni jambo la msingi katika kile tunacholenga kukipata hapa klabuni kwetu”, amesema Brendan.

Kocha huyo wa Liverpool amesema wtaendelea kushuhudia ubora wa Luis Suarez siku zijazo,akiwa ndani ya jezi za Liverpool.

No comments:

Post a Comment