Monday, March 3, 2014

URUSI YASIMAMIA HATUA ZAKE ZA KIJESHI UN.

Urusi imetetea uamuzi wake kutuma wanajeshi nchini Ukraine, katika kikao cha dharura cha baraza la usalama la Umoja wa mataifa.
Balozi wa Urusi katika umoja wa mataifa, Vitaliy Churkin, amesema kuwa rais wa Ukraine aliyeng'olewa madarakani Viktor Yanukovych alikuwa ameiomba Moscow kutuma wanajeshi ili kuwalinda raia na kuzuia vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Akizungumza baada ya mkutano huo wa Baraza la Usalama, Balozi Vitaly Churkin amesema kuwa malalamishi ya bwana Yanukovich yanafanana na yale ya Urusi.
"Nadhani ni muhimu kuzingatia kwamba mtu tunayeamini kuwa ndiye rais halaIi wa Ukraine pia ana wasiwasi tulio nao kuhusu idadi kubwa ya raia wa Ukraine, kuhusu kinachoendelea. Na ametoa wito kwa Urusi kutumia majeshi yetu kuzuia mambo kuwa mabaya zaidi.''
Marekani imesitisha ushirikiano na Urusi.
Lakini balozi wa Ukraine, Yuriy Sergeyev, amesema kuwa madai ya Urusi hayahusiani na kile kinachojadiliwa kwani bwana Yanukovich hakuwa tena rais wa Ukraine.
"Hana lolote kwa sasa. Tukizungumzia hali ilivyo kwa sasa nchini Ukraine na madaraka ya kisheria ya mbunge ambalo lilimng'oa madarakani-hata balozi Churkin hivi leo kama ulisikia alichosema, ametaja kwamba tunaamini hatawahi kuwa rais wa Ukraine. Hii ina kwamba yeye siye mtu wa kuzungumza naye na hana lolote la kuzingatiwa."
Marekani imejibu kwa kusitisha mazungumzo ya kibiashara pamoja na uekezeji kati yake na Urusi, na idara ya Ulinzi ya Pentagon imetangaza kuwa ushirikiano wote wa kijeshi kati ya Marekani na Urusi ikiwemo mazoezi ya kijeshi, ziara za bandarini na mikutano ya mipango yote imesitishwa.

No comments:

Post a Comment