Monday, April 30, 2012

CHARLES TAILOR ANAHATIA-MAHAKAMA.


Mahakama ya kimataifa ya makosa ya Jinai iliyoundwa maalum na umoja wa matifa kwa ajili ya kushughulikia makosa ya uhalifu wa kivita kwa kuwapa silaha waasi wa Sierra Leone kwa malipo ya almasi katika vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor  . Hii ni mara ya kwanza kwa mahakama hiyo maalum iliyoundwa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Sierra Leone kutoa hukumu hiyo.

Jaji Richard Lussick aliyekuwa akisimamia jopo la majaji alisema mahakamani "Mahakama imemkuta na hatia ya kusaidia na kuchochea uhalifu wote huu," akiongeza kuwa Taylor atahukumia adhabu Mei 30.
Taylor, mwenye umri wa miaka 64, alikutwa na hatia ya kusaidia waasi wa Sierra Leone kuendesha kampeni ya uhalifu dhidi ya watu nchi hiyo wakati wa miaka 10 ya vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyouwa watu wapatao laki moja ya elfu 20.

Taylor alilipwa na waasi hao kwa madini ya alhamisi yaliyokuwa yakichimbwa kinyume cha sheria na waasi wa kundi la Revolutionary United Front (RUF) ambao walijulikana kwa mauaji, ubakaji na kukata watu mikono au miguu kwa mapanga.
Taylor alisafirishwa kutoka Freetown kwenda katika mahakama hiyo maalum nje kidogo ya the Hague mwaka 2006 katika kesi ambayo ilikuwa na mashahidi kama vile mwanamitindo wa kimataifa Naomi Campbell na mcheza sinema Mia Farrow kutoka Marekani.(VOA)

No comments:

Post a Comment