Sunday, April 8, 2012

JOYCE BANDA AAPISHWA KUWA RAIS MALAWI.






LILONGWE-MALAWI,
Siku mija baada ya kutangazwa rasmi kwa kifo cha aliyekuwa rais wa Malawi bw.Bingu wa Mutharika makamu  wa rais wa malawi mama Joyce Banda ameapishwa rasmi na kuwa rais wa nchi hiyo;
Bi Joyce banda anakuwa mwanamke wa kwanza kuwa Rais katika ukanda wa Kusini mwa Sahara baada ya Bi.Helen Johnsen wa Leberia Magharibi mwa Afrika.
kabla ya kuapishwa kwake kulikuwa na hofu kuwa pengine wafuasi wa Marehemu Mutharika wangebadili katiba na kumwapisha kaka wa marehemu Ndugu.Peter Mutharika kutokana na Bi. Banda kufarakana na rais mwaka 2010 na kufukuzwa kutoka katika chama cha DPP na kuunda chake cha People's Party.
Mwanamke huyo alishangiliwa kwa nguvu kabla na wakati wa kuapishwa ndani ya ukumbi wa bunge huko Lilongwe.
Bingu Mutharika alifariki hapo jana kutokana na matatizo ya Moyo. 

No comments:

Post a Comment