Monday, April 30, 2012

HATIMA YA KUVUNJWA KWA BARAZA LA MAWAZIRI TANZANIA-MAWAZIRI WAGEUKA MABUBU.

Dar Es Salaam-Tanzania.


Siku chache baada ya kamati  kuu ya chama cha mapinduzi (CCM) kubariki kuchukuliwa hatua kwa mawaziri waliohusishwa na kashfa mbalimbali za kushindwa kuwajibika na matumizi mabaya ya mali za umma, mawaziri wanaoshinikizwa kujiuzulu wamegoma kutoa matamko yao huku wakisema kuwa hatima yao ipo mikononi mwa rais na wengine wakisema wao hawawajibiki kwa kamati hiyo ya chama.

Waziri wa fedha Mustafa Mkulo amenukuliwa na gazeti moja linalotoka kila siku akisema hana la kusema ingawa amedai pi hawajiki kwa kamati ya chama hicho ila serikali, huku mawaziri Maige, Omary Nundu, Nyalandu na George Mkuchika wao hawakuwa tayari kuongea kwa madai hawana la kusema.

Mawaziri hao wamekaa kimya bila kuonekana kama wanania ya kujiuzulu licha ya mashinikizo yote hayo huku wakisisitiza kuwa wao ni watu safi wasio na tuhuma.

No comments:

Post a Comment