Saturday, December 22, 2012

BARAZA LA USALAMA-UN LAIDHINISHA UVAMIZI WA KIJESHI MALI

NEW YORK-MAREKANI,Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa UN kwa pamoja wameidhinisha azimio la kupeleka vikosi vya kigeni kaskazini mwa Mali ili kupambana na Makundi ya kiislamu yenye msimamo Mkali yanayoshikilia eneo hilo tangu mwezi machi mwaka huu

Azimio hilo limepitishwa na Wanachama kumi na tano wa Baraza la usalama la umoja huo na kutoa muda wa kuchukua hatua za lazima kusaidia Serikali ya Mali kurudisha maeneo yanayokaliwa na Wapiganaji wa Kiislamu.

Hata hivyo pamoja na kupitishwa kwa Azimio hilo, Baraza limetaka kufanyika mazungumzo kati ya serikali na makundi ya wapiganaji ili kupata suluhu ya kisiasa nchini Mali.

Mataifa ya Afrika magharibi yamesema tayari yana vikosi 3300 vilivyo tayari kuingia Mali, kulijengea uwezo jeshi la Mali na kusaidia Operesheni za kijeshi nchini humo.
Kwa mujibu wa ripoti ya UN, takribani watu 400,000 wamepotea tangu kuzuka kwa machafuko hayo mwezi machi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment