Friday, December 21, 2012

LEMA ASHINDA RUFAA YA UBUNGE

Mbunge Godbless Lema akiwahutubia wafuasi wake baada ya Hukumu.



DAR ES SALAAM-TANZANIA,Mahakama ya Rufani ya Jijini Dar es Salaam, imemrejea ubumbe, mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema (Chadema).    Lema alieyechaguliwa kuwa Mbunge kwa tiketi ya Chadema, katika uchaguzi mkuu uliopita, ubunge wake ulisita baada ya kuvuliwa na Mahakama Kuu Kanda ya Arusha, Aprili 15, mwaka huu, katika kesi ya kupinga ushindi wake iliyopelekwa mahakamani na baadhi ya wana-CCM.Kwa mujibu wa hukumu imeangalia haswa swala la Locus Stand ya kama waliofungua kesi walikuwa na haki kisheria ya kufanya hivyo.Hivyo kwa kina imeonekana kuwa kadiri ya pingamizi ya mawakili wa lema kimomogoro na Tundu Lissu,waliofungua shitaka dhidi ya lema hawakuwa na locus stand ya kufanya hivyo.kwa hiyo mengine yote yanakuwa null and void.Hukumu hiyo imechukua muda usiozidi nusu saa.kwa hiyo kwa taarifa hiyo Lema amerudi kuwa mbunge halali wa Arusha kuanzia leo.
Taarifa rasmi itaendelea kutolewa hapa Anga za Kimataifa kwa kadiri ya vyanzo vyetu.
(CHANZO:MJENGWA BLOG).

No comments:

Post a Comment