Tuesday, December 18, 2012

JACOB ZUMA ASHINDA TENA UCHAGUZI ANC.


Jacob Zuma
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amechaguliwa tena kuongoza chama tawala nchini humo cha ANC baada ya kupata kura 2.983 dhidi ya 3.977 ya kura zilizopigwa, ikiwa ni ishara ya kumfagilia njia ya kuelekea kwenye uchanguzi wa rais mwaka 2014.

Makamu wa rais wa Afrika Kusini Kgalema Motlenthe ambae awali alitangaza kuwania nafasi hiyo ameonekana kuanguka kisiasa baada ya kuchukuwa uamuzi huo na mwishowekujiondowa ili aendelee kukalia kwenye nafasi yake, ambayo sasa ameikosa.
Cyril Ramaphosa, mfanyabiashara maharufu nchini humo amechukuwa nafasi ya makamu mwenyekiti wa chama, na kumrithi Motlanthe. Cyril Ramaphosa, ni mtu wa karibu sana na rais Zuma na huenda akawa mrithi wa zuma katika chaguzi zijazo, iwapo Jacob Zuma ataamua kutowania muhula mwingine
Zuma alipewa nafasi ya kushinda uchaguzi huo, licha ya kukabiliwa na kashfa mbalimbali na suala la kukigawa chama hicho, kwani asilimia kubwa ya wajumbe wakuu wa chama hicho wanamuunga mkono.
Akiwahutubia wajumbe hao zaidi ya elfu nne siku ya jumapili iliopita, Jacob Zuma aliahidi kupiga vita suala la kukigawa chama na rushwa inayo kithiri ambapo mwenye amehusishwa kutumia vibaya mali ya umma kwa manufaa yake binafsi.
Mbali na hayo Zuma aliahidi pia kupambana na hali ya mgawanyiko katika chama na mzozo uliotikisa nchi hiyo kufuatia mgomo wa wafanyakazi wa migodini uliopelekea watu zaidi ya sitini kupoteza maisha.
Jacob Zuma ametetea utawala wake huku akiahidi kuboresha zaidi na kutia kipao mbele masuala ya elimu, kuopiga vita rushwa na kupiga vita wawindaji haramu wa mifugo ya vifaru.
Wajumbe wa chama cha ANC walianza kukutana tangu siku ya Jumapili iliopita huko Bloenfontein na kutamatisha kikao hicho baada ya kuwapata viongozi hao wapya.(CHANZO:RFI)

No comments:

Post a Comment