Saturday, December 8, 2012

KENYA,TANZANIA,UGANDA WAFUNGUA MIPAKA KWA WATAALAMU

ARUSHA-TANZANIA

Nchi tatu za Afrika Mashariki Tanzania, Kenya na Uganda zimekubaliana kutambua makubaliano kuhusu watalaamu wa kiufundi yatakayowaruhusu watalaamu hao kuingia na kufanya kazi wakiwa huru katika nchi hizo.

Hafla ya kusainiwa kwa makubaliano ilifanyika mjini Arusha Tanzania.
Burundi na Rwanda ambazo pia ni wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki hazikushirikishwa kwenye makubaliano hayo kutokana na ukosefu wa watalaamu wa kiufundi katika nchi zao.

Akizungumzia hatua hiyo, mkurugenzi wa miundo mbinu wa Afrika Mashariki Bw Philiph Wambugu amesema makubaliano hayo ni chombo muhimu cha utekelezaji wa soko huria la pamoja ambalo linafikia mwaka wake wa tatu tangu lianzishwe mwaka wa 2010.(CHANZO:TEHRAN)

No comments:

Post a Comment