Friday, March 29, 2013

GHOROFA LAANGUKA DAR ES SALAAM-WATATU WAFA,MAMIA WAKWAMA CHINI.

DAR ES SALAAM-TANZANIA,
Mamia ya wafanyakazi wa ujenzi wanahofiwa kukwama ndani ya jengo lenye ghorofa kumi na mbili lililoanguka mapema leo mjini Dar es Salaam.
"Nilidhani lilikuwa tetemeko la ardhi, na kisha nikasikia mayowe,". "
- shuhuda
Kulingana na walioshuhudia ajali hiyo, watu walisikika wakipiga mayowe kutaka msaada.

"nilidhani lilikuwa tetemeko la ardhi, na kisha nikasikia mayowe,'' alisema shahidi mmoja.

Jengo hilo liko katikati mwa Dar es Salaam na lilianguka saa tatu kasorobo asubuhi kwa saa za afrika mashariki.
Mamia ya watu wanaaminika kuwa ndani ya jengo hilo huku wengine wakiwa nje wakati wa ajali hiyo . Hata hivyo idadi kamili ya watu hao bado haujulikani.











No comments:

Post a Comment