Thursday, March 21, 2013

OBAMA KUZULU PALESTINA LEO.


 


Ramalla-Palestina,
Baada ya kuwasili Israel hapo jana Rais wa Marekani Barack Obama atakuwa na ziara ya nchini Palestina leo na kufanya mazungumzo na rais wa Palestina Bw.Mahmoud Abbas.Mazungumzo ya Obama na Abbas yataangazia zaidi mzozo wa amani kati Palestina na Israel ambao kwa muda mrefu haujapata suluhu.

Obama anazuru Ramalla kwa saa kadha kabla ya kurejea Bethlehem kutoa hotuba kwa raia wa Israel kuhusu uhusiano kati ya Israel na Palestina na mchango wa Marekani kuhakikisha kuwa amani inadumu katika eneo hilo la Mashariki ya Kati.

Hata hivyo, raia wa Palestina wanasema hawaoni umuhimu wa ziara ya Obama katika Mamlaka hiyo kwa kile wanachokisema kuwa tangu rais huyo wa Marekani alipoingia madarakani hajawafanyia chochcote .

Ziara ya Obama inakuwa ni ziara yake ya kwanza kwenye eneo la Mashariki ya kati tangu kuchaguliwa kwake kwa muhula wa pili kama kiongozi wa taifa hilo lenye nguvu zaidi duniani.

Obama amemwambia Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu kuwa ,Marekani haina rafiki wa dhati kama Israel na itaendelea kujenga uhusiano thabiti kati ya mataifa hayo mawili.

Kuhusu Iran rais Obama amesema kuwa nchi hiyo ina nafasi ya kujirekebisha kuhusu mpango wake wa Nyuklia kupitia njia za kidiplomasia kuepuka nguvu za kijeshi kutumiwa dhidi yake.

No comments:

Post a Comment