Tuesday, March 19, 2013

MAREKANI YARUSHA NDEGE ZA B52 KOREA KUSINI-NI TISHIO KWA KOREA KASKAZINI.


b52h-strategic-bomber
Ndege aina ya B52 ikiwa hewani

Kabla ya kuruka

SEOUL-KOREA KUSINI,
Marekani imerusha ndege zenye uwezo wa kuzuia mabomu ya Nyuklia na kubeba silaha nzito katika kile ilichoelezea kama itikio kwa vitisho vya Korea ya Kaskazini ambayo hivi karibuni imetishia kuishambulia.
"Tunaonesha uwezo kuwa tumepanua uwezo ambo ni muhimu dhidi ya tishio la Korea Kaskazini" Alisema msemaji wa Pentagon Bw. George Little.

Marekani imeonekana kutilia maanani tishio la hivi karibuni la Korea Kaskazini, ambapo hivi karibuni ilipitisha bajeti ya zaidi ya trilioni 1.5 kuboresha mitambo yake ya kutungua makombora makubwa yakiwemo ya Nyuklia huko iliyopo katika ardhi yake kama kinga dhidi ya shambulizi lolote, hali ambayo ni changamoto kwa Korea Kusini na Japan ambao pia ni maadui wa Korea Kaskazini.

No comments:

Post a Comment