Tuesday, March 26, 2013

MAJESHI YA KOREA KASKAZINI YAJIWEKA TAYARI KUSHAMBULIA KUSHAMBULIA KAMBI ZA JESHI LA MAREKANI MJINI HAWAI NA GUAM.

 

PYONGYANG-KOREA KASKAZINI,
Serikali ya Korea Kaskazini imetangaza kuviweka tayari vikosi vyake kwenye mstari wa mapambano tayari kwa mashambulizi dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani za mjini Hawaii na Guam pamoja na Kora Kusini.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa shirika la utangazaji wa Korea Kaskazini, imesema kuwa amri imetolewa na kamanda mkuu wa majeshi ya nchi hiyo ambayo inawataka wanajeshi wote kuwa mstari wa mbele tayari kwa kusubiri amri ya kutekeleza mashambulizi dhidi ya Marekani.


Tangazo hilo la Serikali ya Korea Kaskazini linakuja wakati ambapo nchi ya Korea Kusini na Marekani zimemaliza mazoezi ya pamoja ya kijeshi ambayo Korea Kaskazini ilidai kuwa ni uchokozi dhidi ya taifa lao.


Hii si mara ya kwanza kwa Korea Kaskazini kutangaza kutishia kuishambulia nchi ya Marekani ambapo imeapa kutumia silaha za Nyuklia kutekeleza mashambulizi yake dhidi ya maadui zake.

Picha za video zimemuonesha kiongozi wa taifa hilo Kim Jong Un akitembelea kambi za wanajeshi wa nchi hiyo ambao wamekuwa kwenye mazoezi ya kijeshi kujiweka tayari kuilinda nchi yao.

No comments:

Post a Comment