Monday, March 11, 2013

MTUHUMIWA MKUU WA UBAKAJI INDIA AJINYONGA GEREZANI

Mwili wa Singh ukitolewa gerezani .
Ram Singh 
DELHI-INDIA, Mtuhumiwa  katika kesi ya ubakaji wa msichana mmoja wa chuo kikuu ambaye baadaye alifariki nchini India, amekutwa akiwa  amefariki ndani ya gerezanila Tahir nchini India  alipokuwa akishikiliwa.

Kwa mujibu wa polisi wamesema kuwa Ram Singh, alijinyonga akiwa ndani ya gereza la Tihar mjini Delhi's Tihar, ingawa mawakili wa utetezi wanadai kuwa huenda alinyongwa.
Ram Singh, aliyekua na umri wa miaka 33, alikuwa mmoja wa washukiwa katika kesi ya ubakaji wanaozuiliwa na polisi kwa madai ya mauaji ya msichana waliyembaka.
Wote walikanusha madai hayo.

Shambulizi dhidi ya mwanafunzi huo, lililofanyika Desemba mwaka jana, lilizua mjadala mkali nchini India kuhusu udhalilishwaji na ukatili dhidi ya wanawake.

Washukiwa wengine wa ubakaji bado wanazuiliwa katika gereza hilo.Kesi ya mshukiwa wa sita inaendeshwa katika mahakama ya watoto.

Mwandishi wa BBC Sanjoy Majumder,mjini Delhi,amesema kuwa kifo cha bwana Singh kinakuja kama aibu kubwa kwa maafisa ambao wanakabiliwa na shinikizo kubwa kuhusu kesi hiyo.
Msemaji wa jela hiyo Sunil Gupta, aliambia BBC kuwa Ram Singh alijinyonga kwa banketi usiku wa kuamkia leo.(CHANZO:BBC)

No comments:

Post a Comment