Thursday, March 7, 2013

MWILI WA RAIS HUGO CHAVEZ WAAGWA-KUZIKWA IJUMAA

Mwili wa Marehemu Hugo Chavez katika gari.






Maelfu ya raia wa Venezuela wakiusindikiza mwili wa aliyekuwa rais wao.






Mwili wa Chavez umelazwa katika kituo cha mafunzo ya kijeshi mjini Caracas na marais wa nchi jirani walifika kutoa heshima zao za mwisho akiwemo Rais wa Bolivia Evo Morales na mwenzake wa Argentina Cristina Fernandez de Kirchner.
Add caption




Mwili wa aliyekuwa rais wa VEnezuela Bw. Hugo Chavez, Umepitishwa kwenye umati mkubwa wa wafuasi wake katika mitaa ya mji mkuu Caracas kuagwa na wafuasi na wananchi wa nchi hiyo.Kwa sasa  mwili huo umelazwa katika kituo cha mafunzo ya jeshi katika mji mkuu Caracas.
Watu wengi waliangua kilio huku wakichukua picha za kiongozi wao aliyefariki dunia .Mama yake na watoto wake walikusanyika mbele ya jeneza kutoa heshma zao .
Katika shughuli hiyo iliyoongozwa na makamu wa rais wa nchi hiyo Bw.Nicolas Maduro.


Mwili wa rais Chavez umepelekwa katika chuo cha kitaifa cha mafunzo ya kijeshi ambapo utazikwa kesho Ijumaa.
Bwana Chavez alifariki akiwa umri wa miaka 58 baada ya kuugua Saratani kwa zaidi ya miaka miwili.
Maelfu ya watu awali walikwenda barabarani mjini Caracas kutoa heshima zao za mwisho kwa Chavez wakifuatana na gari lililokuwa limebeba jeneza lake kuelekea katika chuo cha mafuzno ya jeshi.
Mazishi ya kitaifa ya Chavez yatafanyika Ijumaa.
Mkuu wa ulinzi wa Rais alinukuliwa akisema kuwa alikuwa na bwana Chavez alipofariki.
Generali Jose Ornella, alisema kuwa Chavez alifariki kutokana na mshtuko wa moyo na katika siku zake za mwisho kabla ya kifo cha ealisema angependa kuendelea kuishi.
Jeneza lake lililokuwa limefunikwa bendera ya nchi hiyo uliwekwa katika ukumbi ambao ni kumbukumbu ya waliopigania uhuru wa watu wa Amerika ya Kusini
Maelfu ya watu walipanga foleni kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu Chavez, wakiwemo maafisa wa serikali na viongozi wa Amerika ya Kusini,kama Rais wa Bolivia Evo Morales na Rais wa Argentina Cristina Fernandez de Kirchner.

No comments:

Post a Comment